Jumatano, 9 Julai 2014

KUTANA NA NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI MPYA - JENISTA MHAGAMA


Nilimfahamu muda mrefu tangu akiwa kama mwalimu pale Peramiho Girls. Kukurukakara zake za kupigania haki za walimu kuanzia alipokuwa mwalimu, kisha UWT hadi kuwa mbunge wa Peramiho, zimeonekana kwa kiasi kikubwa, hata sasa kuteuliwa kuchukua nafasi ya Phillip Mulugo kama Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Tanzania.
Kuteuliwa kwake katika nafasi hii kumenipa faraja kwa kuwa utekelezwaji wa mpango wa "Matokeo Makubwa Sasa' katika sekta ya elimu unaweza ukaangaliwa kwa jicho la uzoefu zaidi katika kuhakikisha kwamba walimu wanapewa haki zao kama inavyotakiwa kwa kuwa Mheshimiwa Jenista Mhagama naye amepitia njia hiyo hiyo.
Pia, sote tunafahamu misimamo yake mikali awapo bungeni hasa katika utekelezaji wa mikakati yenye manufaa kwa wananchi. Nina imani kubwa kuwa Wizara ya Elimu haitakuwa kama ilivyokuwa kwa miaka yote ya nyuma. Jambo moja tu ambalo nadhani mheshimiwa Rais JK angeliangalia kwa jicho la ziada, ni kwamba Wizara nzima ingevunjwa na mfumo wake ujengwe upya, kuanzia Waziri Dkt shukuru Kawambwa mpaka makatibu wa Wizara na watendaji wake ambao wamekaa Wizarani kwa muda mrefu bila kuwa na matunda mazuri. 
Nina imani uchapakazi wa mheshimiwa Jenista Mhagama utafunika udhaifu wa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi mheshimiwa Dkt Shukuru Kawambwa.
Weka maoni yako hapa!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni